JPM AMWAGA MKWANJA KWA WAISLAMU
Rais John Magufuli amemwaga burungutu la fedha kusaidia Waislamu ambao watakwenda kuhiji Agosti mwaka huu.
“Najua kuna Waislamu watakwenda kuhiji nadhani Agosti, naomba kama inaruhusiwa na mimi nichangie kitu kidogo kadri ya uwezo wangu, nimejipigapiga na mimi nikaona nichangie kitu kidogo, kana inaruhusiwa naomba Mufti uje nikukabidhi,” alisema Magufuli alipokuwa akizungumza katika Baraza la Eid el Fitri jijini Dar es Salaam jana.
Baada ya kutamka maneno hayo, alishika begi dogo kama briefcase akampa msaidizi wake ambaye alilifungua na kuchomoa burunguti la noti na kumkabidhi Mufti, Sheikh Mkuu Zubeiry Ally. Hata hivyo haikufahamika kiasi cha fedha hizo.
Kabla ya kutoa fedha hizo, awali akimkaribisha Rais Magufuli kuhutubia, Mufti Zubeiry aliwataka Waislamu kutumia Bakwata katika safari za hija zitakazogharimu Dola 3,800 kwa mtu mmoja.
Labels: Breaking News
0 Comments:
Post a Comment
Nawapenda
Subscribe to Post Comments [Atom]
<< Home